• Breaking News

    VIPINGAMIZI VYA KUKUA KWA MKRISTO

    Vipingamizi  ni visababishi au vitu vinavyomfanya mkristo asiweze kukua kiroho katika ukristo
    Mstar wa msingi,Efeso 6:10_12 Biblia inasema( 10_  Hatimaye mzidi kuwa hodari katika Bwanana katika uwezo wa nguvu zake,11_vaeni siraha zote za Mungu mpate kuzipinga hila za shetani)
    Pia Yakobo 4:7 Biblia unasema(4:7_ Kwahiyo jinyenyekezeni kwa Mungu mpingeni shetani naye atawakimbia) Mwandishi ni Yakobo ambaye inawezekana ikawa ni yule ndugu wa Yesu au yule Yakobo aliyekuwepo Jerusalem, Matendo 15:13(Na hao walipokwisha kunyamaza Yakobo akajibu akisema Ngugu zangu nisikilizeni)
    Barua ya Yakobo juu ya kumpinga shetani si kwa mtu  binafsi Bali kwa watu wa Mungu wote, 
    Tunaona pia Yesu aliendelea kukua  katika Hekima ya kumpendeza Mungu,Luka 2:52(52_Naye Yesu akazidi  kuendelea katika Hekima na kimo akimpendeza Mungu na wanadamu
    Vipingamizi vinavyofanya watu kutokua kwa mkristo pamoja na
    1.Kutomtii Mungu,kukataa kujiweka chini ya Mungu, kutomtii Mungu kunasababisha kutokuwa kiroho ata hivyo Mungu anataka tutiii, Yakobo 4:7( kwahyo jinyenyekezeni kwa Mungu,Mpingeni shetani naye atawakimbia) ,Efeso 6:12 kwa maaña kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama Bali ni juu ya falme na mamlaka,juu ya wakuu wa giza hili,juu ya mapepo wabaya katika ulimwengu wa roho ,1 Petro 8_9(8_kuweni macho ;kesheni! maaña adui yenu ibilisi huzungukazunguka kama simba aungurumaye akitafuta mawindo 9_ Muwe imara katika imani nkijua kwamba ndugu zenu pote duniani wanapatwa 
    na mateso hayohayo) kwahyo  tunapaswa kutii kwa Mungu  ili tuweze kukua rohoni ata tukaweze kumpinga adui shetani

    2 kutompinga shetani,Biblia inataka kumpinga shetani pamoja na kazi zake tunaona katika Efeso 6:11(11_Vaeni siraha zote za Mungu mpate kuweza kupinga hila za shetani) ivyo basi ili kukua  kiroho tunatakiwa  kuvaa siraha za kupambana ili tuweze kushinda vita na majaribu ya shetani, siraha za kiroho inaweza ikawa MAOMBI,mfungo NK


    Kutomkaribia Mungu, Ezekiel 1:3(3_Neno la Bwana lilimjia Ezekieli,kuhani mwana wa Buzi,kwa dhairi katika nchi ya wakaldayo karibu na mto kebari,na mkono wa Bwana ulikuwa apo juu yake) Mika6:6_8(6_Nimkaribie Bwana na kitu gani,na kuinamama mbele  za Mungu aliye Juu je Nimkaribie kwa sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka 7_Je Bwana atapendezwa na kondoo elfu za kondoo waume,au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu,mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu?8_Ee mwanadamu yeye amekuonyesha yaliyo mema ,na Bwana anataka nini kwako,ila kutenda haki, na kupenda rehema na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!


    ILIKUKUA KIROHO , tunatakiwa kumtanguliza Mungu katika maisha  yako, Mathayo6:33(Bali utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo yote mtazidishiwa,Rumi 14:17(17_maaña ufalme wa Mungu si Kula wala kunywa,Bali ni haki na amani na furaha katika roho mtakatifu) 1 wafalme 3:13_14(13_Na mambo yale usiyoyaomba nmekupa,Mali na fahari, hata hapatakua na mtu katika ufalme kama wewe siku zako Aye)




    Asantekwa usomaji somo hili limeandaliwa na mchungaji Kikoti TAG ulanda
    O768333841
    Pia unaweza kufatilia masomo kama aya KILA siku katika  GodloveApp (http//goo.gl/pRBmJp)karibu wote

    1 comment: