• Breaking News

    JINSI NA MAANA YA KUOKOKA

    Utangulizi wa somo hili letu, kwanza tunatakiwa kujua, kuna aina mbili za wahubiri na watumishi wa Kikristo, watazamiao mabaya na walio yakini wenye mashaka na wasio amini
    Kuna baadhi ya watu hukiri kwamba kama wakihubiri kwenye njia za miji  hakuna mtu atakayewasikiliza na wahitaji wa Neno watawadhihaki( watawacheka)
    Tunaamini kuwa tunapohubiri kwenye njia za miji watu watakusanyika na kutuzunguka wakijitaidi  kisikiliza ujumbe wetu na hata wapitaji watafurahia kuona mkristo akishuhudia
    Biblia inasema sisi tumepita mautini na kuingia uzimani 1Yohana 3:14" sisi tunajua kwamba tumekwisha kupita kutoka katika kifo na kuingia katika uzima kwa sababu tunawapenda ndugu zetu, mtu asiye na Upendo ubaki katika kifo " Twende moja kwa moja katika somo  letu,lina vipengele kama vifuatavyo


    A.Maana ya kuokolewa/Tunaokolewaje

    Tunaokolewa kutoka dhambini 1Timotheo 1:15"usemi huu ni wakuaminika na wakufaa kukubalika kabisa,Kristo Yesu  alikuja ulimwenguni kuwaokoa wenye dhambi, Nani mkosefu kuliko hao wote"
    Md 2:21" Hapo yeyote atakaye omba kwa jina la Bwana  ataokolewa
    Yohana 3:17" Maana Mungu hakumyeye  Mwana ulimwenguni ili auhukumu Ulimwengu,Bali Ulimwengu uokolewe katika yeye

    B Kuokoka maaña yake Nini

    1.Kuokoka ni kuzaliwa kwa roho geuka kuwa mtoto wa Mungu,kuzaliwa mara ya pili    Yohana 3:1_8"Bali palikuwa na mtu mmoja wa mafarisayo,Jina lake Nikodemo ,Mkuu wa wayahudi 2Huyo alimjia usiku,akamwambia Rabi twajua kwamba u mwalimu, umetoka kwa Mungu, kwa maaña hakuna mtu awezaye kufanya ishara kama hizi uzifanyazo wewe,isipokuwa Mungu yu pamoja nawe, 3 Yesu akajibu akamwambia amini amini nakuambia mtu asipozaliwa Mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu,4 Nikodemo, akamwambia,awezaje mtu kuzaliwa akiwa mzee, aweza kuingia tumboni mwa mamaye Mara ya pili akazaliwa, 5 Yesu akajibu, Amino,amini nakuambia mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia ufalme wa Mungu, 6 kilichozaliwa kwa mwili ni mwili na kilichozaliwa kwa Roho ni roho, 7 usistaajabu kwa kuwa nirikwambia,Hamna budi kuzaliwa Mara ya pili, 8 Upepo uvuma upendako na sauti yake waisikia,lakini hujui unakotoka wala unakokwenda ,kadhalika na Hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa roho"
    Kwahiyo unapookoka upokei dini Bali unampokea kristo   Yohana 1:12" Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu ndio wale walioliamini jina lake"    Yohana 3:7" usistaajabu kwa kuwa nilikwambia ,Hamna Budi kuzaliwa Mara ya pili"
    2.Ni kusamehewa dhambi                                                  Zaburi 103:3 " akusamee maovu yako yote ,akuponye magonjwa yako yote"   Mathayo 1:21"Naye atazaa mwana, naye atamwita jina lake Yesu,maana yake ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi"   Isaya 43:25 "Mimi, naam,Mimi,ndimi nayefuta makosa yako kwa ajiri yangu mwenyewe"      Waebrania 10:17" sitakumbuka tena dhambi zao wala vitendo vyao vya uharifu"

    3. Kuokoka ni kupokea uhai mpya,     2Wakorinto 5:17"Hata imekuwa mtu akiwa ndani ya Kristo ,amekuwa kiumbe kipya,ya kale yamepita tazama yamekuwa mapya"     Yohana 10:10" Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; Mimi nilikuja ili wawe na uzima kisha wawe nao tele"

    4.Ni kupokea amani        Yohana  14:27" Amani nawaachieni ,Amani yangu nawapa,niwapavyo Mimi sivyo kama Ulimwengu  utoavyo,msifadhaike moyoni mwenu wala msiwe na woga"      Isaya 57:21" Hapana amani kwa wabaya; Asema Mungu wangu"

    5.Unapookoka unapewa ushirika na Baba      Yohana 1:3vyote vilifanyika kwa huyo wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika"  Mathayo 18:24, "Alipoanza kuifanya aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi"     Isaya 59:2" Lakini maovu yenu yamewafarakanisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha USO wake usionekane,Hata ataki kusikia"    Matendo 26:28" Agripa akamwambia Petro kwa maneno wachache Wadhani wanifanya Mimi  kuwa mkristo "      1Yohana 1:9 Kulikuwapo Nuru alisi amtia nuru KILA mtu akija katika ulimwengu "
    Yesu alisema aniaminiye na kubatizwa ataokoka asiye amini ataukumiwa(Marko 16:16)
    Kwahiyo unatakiwa kumwamini Yesu kristo katika maisha yako
    Unatakiwa kumkiri Yesu kwa kinywa chako ili kutubu kwake na si kwa mtu mwingine   Warumi 10:9" Kwa sababu unamkiri Yesu kwa kinywa chako yakuwa Bwana na kuamini moyoni mwako yakuwa Mungu alimfufua katika wafu Utaokoka"  Yaani wewe baba, kijana mama, binti na watu wote ,
    Hizo zote ni maana na jinsi ya kuokoka, Mungu akubariki mpendwa na udumu katika wokovu👍👍👊
    Somo ili limeandaliwa na mchungaji kikoti, Ulanda TAG  0768333841
    Pia masomo kama haya ya kila siku yanapatikana katika blogi hi pia unaweza Kutupata katika GodloveApp unaweza kudownload katika link(http://goo.gl/pRBmJP)


    No comments