• Breaking News

    JINSI IMANI INAVYWEZA KUKUA

    Imani ni nini_ ni kuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo, bayana ya mambo yasiyoonekana(Waebrania11:1)
    Imani huja kwa kusikia Neno la Mungu,  Warumi 10:17" Basi imani chanzo chake ni kusikia na kusikia Huja kwa Neno la kristo"
    Lazima tugundue jinsi imani inavyoweza kukua katika maisha ya mwamini/hata asiye mwamini.Tunakuwa Imani hata imani utukufu hadi utukufu

    VITU 5 KWA AJIRI YA UKUWAJI WA IMANI
    Imani inafananishwa na mbegu
    1.mbegu lazima iwe na chakula, udongo wenye rutuba, maji na mwanga wa jua
    Vitu ivi👆👆👆 ni muhimu na lazima sana katika ukuwaji wa mbegu
    (a) Udongo ni kusikia Neno  la Mungu,  Warumi 10:17" Basi imani chanzo chake ni kusikia na kusikia  huja kwa Neno la Kristo "   Ezekiel 33:7" Basi wewe mwanadamu nimekuweka kuwa mlinzi wa Israel basi ulisikie neno hili kinyani mwangu  ukawape maonyo yangu"
    (b)Maji_ kutii Neno la Mungu  kwahiyo lazima tuelewe  Paulo anaposema  imani chanzo chake ni kusikia, Ni kusikia kile ambacho MUNGU anasema kwako na kutenda kile unachokisikia ,    Yakobo 1:22" msijidanganye wenyewe kwa kisikiliza  tu Neno  lake Bali litekelezeni kwa vitendo"   Kumb 28:1_15" itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana,MUNGU  wako,kwa bidii kutunza,kufanya maagizo yake yote nikuagizayo Leo, ndipo Bwana Mungu wako atakapokutukuza juu ya mataifa yote duniani,2 Na Baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana,MUNGU wako, 3 utabarikiwa mjini,utabarikiwa mashambani, 4 utabarikiwa uzao wa tumbo lako,na uzao wa nchi yako,na uzao wa wanyama wako na kondoo zako, 5 litabarikiwa kapu lako na chombo chako cha kukandia unga, 6 utabarikiwa uingiapo utabarikiwa utokapo, 7 Bwana utawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako, watakutokea kwa njia moja,lakini watakimbia mbele yako kwa njia Saba, 8 Bwana ataiamuru Baraka ije juu yako katikusipo zako na mambo yote utakayotia mkono wako, 9 Bwana atakuweka kuwa taifa Takatifu kwake kama alivyokuapia,utakaposhika maagizo ya Bwana Mungu wako na kutembea katika njia zake, 10 Na mataifa yote ya dunia yatakuona umeitwa kwa jina la Bwana nao watakuwa na hofu kwako, 11 Bwana atakufanya uwe na wingi wa uheri,katika uzao wa tumbo lako na uzao wa wanyama wako wa mifugo na uzao wa nchi yako, katika nchi ya Bwana niliyowaapia Baba zako kwamba atakupa, 12 atakufunulia Bwana hazina yake nzuri nayo ni mbingu, kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake na kwa kubarikia kazi yote ya mkono wako, 13 Bwana atakufanya kuwa kichwa wala si mkia, nawe utakuwa juu tu wala si chini, utakapoyasikia maagizo ya Bwana Mungu wako nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kuyafanya, 14 msipokengeuka katika maneno niwaamuruyo Leo, kwa lolote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto, kwa kuifata miungu mingine na kumtumikia,15 lakini itakuwa usipotaka kuisikia sauti ya Bwana,MUNGU wako,usiyaangalie kufanya  maagizo yake yote na amri zake, nikuagizayo hivi Leo,ndipo zitakapokuja laana hizi zote na kukupata,"
    Mfano baba anaweza kumuita mtoto na yule mtoto akaitika lakini asiende kama alivyosikia kuitwa,
    Swali Je ? Alisikia Neno la baba yake?
    Ki Biblia  hakusikia_kwa sababu akutendea kazi kule kusikia,   Mwanzo 26:5" kwa sababu ibrahimu alinitii Mimi na kuzingatia maagizo yangu na Sheria zangu"
    Hivyo basi tunasema imani ina mambo matatu
    1.Utii
    2.Tendo la kulingana
    3.Kusikia sauti ya MUNGU
    Kwahiyo maaña halisi ya kusikia ni kutendea kazi kile ulichokisikia
    Mungu akubariki mpendwa katika Kristo,
    Somo hili limeandaliwa na mchungaji Kikoti Ulanda TAG, 0768333841
    Pia masomo kama haya ya kila siku unaweza ukayapata katika blogi hi na GodloveApp unaweza kudownload katika link(http://goo.gl/pRBmJp) asante👍👍👊👊

    No comments