• Breaking News

    SIKUKU YA PASAKA

    Andiko_  kutoka 12:2_3, 6_7,12_13, "2_Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu, utakuwa wezi wa kwanza wa mwaka kwenu, 3_ semeni na mkutano wote wa Israel mkawaambie siku ya kumi ya Mwezi huu KILA mtu atatwaa mwana kondoo kwa hesabu ya nyumba ya baba zao,mwana kondoo kwa watu wa nyumba  moja"    kutoka  12:6_8 "6_Nanyi ntaweka ata siku ya kumi na nne ya Mwezi  ule ule ,na kusanyiko lote la mkutano wa Israel watamchinja jioni, 7_ Na watatwaa baadhi ya damu yake na kuitia katika mlimo miwili na katika kizingiti cha juu, katika zile nyumba watakazomla"    kutoka 12:12_13 "12_maaana nitapita kati ya nchi ya misri usiku huu,  Nami nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya misri, wa mwanadamu na wanyama nami nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya misri Mimi ndimi Bwana, 13_ Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba mtakazo kuwamo, nami nitakapo iona ile damu nitapita juu yenu lisiwapate pigo la wote"
    Kitabu cha kutoka ,Mwandishi ni Musa , ujumbe wa kitabu hiki ilikuwa ni UKOMBOZI KUTOKA UTUMWANI , 
                   Maaña ya Pasaka
    Kutoka 12: 2, apo juu 👆👆 tumeona Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi mingine 
    1.pasaka ilikuwa ni ukombozi kwa ajiri ya Israel

    2.pasaka huonyesha surà ya wokovu mkuu, waebrania, Waebrania 2:3 " Basi sisi tutaokokaje kama hatuujui wokovu mkuu kama huu? Kwanza Bwana mwenyewe aliutangaza wokovu huu na wao waliomsikia wakituthibitishia ya kwamba ni kweli"

    3.pasaka huonyesha  ukombozi wetu katika utumwa wa dhambi na vifungo

    Farao  alivaa taji iliyokuwa na nyoka aina ya Kobra kwa mbele yake ,nyoka alikuwa alama ya shetani  Mwanzo 3:1_14 " 1_ Basi nyoka alikuwa mwelevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu, Akamwambia mwanamke Ati! hivi ndivyo alivyosema Mungu msile matunda ya miti yote ya bustani? 2_ Mwanamke Akamwambia  nyoka  matunda ya miti ya bustani twaweza Kula 3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema msiyale wala msiyaguse msije mkafa 4 nyoka Akamwambia mwanamke hakika hamtakufa 5 kwa maaña  Mungu anajua ya kwamba siku mtakapokula matunda ya mti huo  mtafumbuliwa macho Nanyi ntakuwa kama Mungu mkijua mema na mabaya 6 mwanamke alipoona ya kuwa ule mti unafaa kwa chakula,wapendeza kwa  kwa macho nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe naye akala 7 Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajua kuwa wa uchi ,wakashona majani ya mtini watakufanyia nguo 8 " Kisha Bwana Mungu akitembea bustanini wakati wa jua kupunga, Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani,Bwana Mungu asiwaone 9 Bwana Mungu akamwita Adamu Akamwambia uko wapi? 10 Akasema nalisikia sauti yako bustanini nikaogopa kwa kuwa Mimi ni uchi nikajificha  11 Nani aliyekuambia u uchi, Je! Umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza usiyale? 12 Adamu Akasema huyo mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye aliyenipandsha matunda ya mti huo, nikala 13Basi Bwana Mungu Akamwambia mwanamke nini hili ulilolifanya? Mwanamke Akasema nyoka alinidanyanya nikala 14 Bwana Mungu Akamwambia nyoka kwa sababu umeyafanya haya umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote waliokaa mwituni, kwa tumbo utakwenda na mavumbi utakula siku zote za maisha yako"
    Ufunuo  12:9" Yule joka akatupwa ,Yule mkubwanyoka wa zamani aitwaye ibilisi  na shetani, audanganyaye Ulimwengu wote,akatupwa hata nchi,na malaika zake wakatupwa pamoja naye"

    Taji ya farao ilikuwa mfano wa mamalaka katika ulimwengu wa roho juu ya misri , kama vile shetani alivyotawala kupitia farao na Mungu aliamua kuendelea utawala wake kwa kupitia  Musa na fimbo yake , kutoka  4:17 "Nawe utatwaa fimbo hii mkononi mwako na kwa hiyo utazifanya zile ishara"

    Farao asingewaachia watumwa wake bila mapambano ,na Kuwaachia wana wa Israel  alikuwa ameweka masharti juu ya Israel 
    Pasaka ni Mwanzo mpya 
    Ukombozi kutoka dhambini, kama vile pasaka ilivyokuwa mwisho wa utumwa ,nguvu na umaskini ,basi tusheherekee kwa maaña hiyo tunapokuja kwa mwana kondoo wetu Pasaka 
    Tuwe  na mwanzo mpya 

    2 wakorinto 5: 17" lakini vyote pia vyatoka kwa Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo ,naye alitupa Huduma ya upatanisho

    Mathayo 1:21 Naye atazaa mwana ndiye atakayewaokoa watu na dhambi zao"
    1Yohana 3:8 "KILA mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi,kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezakiwa kutokana na Mungu

    Yohana 8:36" Najua ya kuwa ninyi ni uzao wa ibrahimu lakini mnanitafuta kuniua kwa sababu neno langu halipo ndani yenu"





    Somo hili limeandaliwa na mchungaji kikoti  ulanda  TAG, 0768333841
    Pia masomo kama haya ya KILA siku utayapata katika blog hi au application GodloveApp unaweza kudownload kupitia link (http:/goo.gl/pRBmJp) karibu




    No comments